Simba Sports Club
News

Mashabiki 35,000 kuziona Simba, ASEC Mimosas Jumapili

1 Feb 2022

CAF imetaka kufuatwa taratibu zote za kujikinga na ugonjwa wa corona kama kukaa kwa nafasi baina ya mtu na mtu, kuvaa barakoa na kunawa mikono kwa maji safi.

CAF imesisitiza taratibu hizo kufuatwa hivyo kila shabiki anapaswa kuchukua hatua na kumlinda mwenzake aliye karibu yake kwa muda wote wa mchezo.

Advertisement

Uongozi wa klabu umepanga kuhakikisha maandalizi yote yanakamilika na taratibu zote zinafuatwa huku ukiwataka mashabiki kununua tiketi mapema muda ukifika ili kuondoa usumbufu siku ya mchezo.

Back to homepage
Share this story