CAF imetaka kufuatwa taratibu zote za kujikinga na ugonjwa wa corona kama kukaa kwa nafasi baina ya mtu na mtu, kuvaa barakoa na kunawa mikono kwa maji safi.
CAF imesisitiza taratibu hizo kufuatwa hivyo kila shabiki anapaswa kuchukua hatua na kumlinda mwenzake aliye karibu yake kwa muda wote wa mchezo.
Advertisement
Uongozi wa klabu umepanga kuhakikisha maandalizi yote yanakamilika na taratibu zote zinafuatwa huku ukiwataka mashabiki kununua tiketi mapema muda ukifika ili kuondoa usumbufu siku ya mchezo.