Malota amesema katika kipindi chake alikuwa hawazi kabisa kuhusu starehe na anasa hata mahusiano alianza baada ya kufikisha umri wa miaka 25 na hicho ndicho kilimfanya zaidi kuwaza soka muda wote.
Kwenye historia yake ya soka Malota hakuacha kumtaja Zamoyoni Mogela kuwa ndiye aliyewaambia Simba kumsajili na kutengeneza maelewano makubwa (Combination) na tishio kwa mabeki kwenye kikosi chetu.
Advertisement
Fuatilia hadi mwisho mahojiano haya, Malota amefunguka mambo mengi ikiwemo kambi tuliyoweka nchini Brazil, asili ya jina 'Ball Juger' na mengine mengi.