Simba Sports Club
News

LIVE UPDATE: Simba 1-1 Cambiasso

11 Oct 2021

Kikosi cha Simba kinachoanza

Beno Kakolanya (30), Said Noshard(43), Gadiel Michael (2), Erasto Nyoni(18), Henock Inonga (29), Jonas Mkude(20) Hassan Dilunga (24), Mzamiru Yassin (20) Jimmyson Mwanulke(27), Ibrahim Ajib (10) Bernard Morrison (3).

Kikosi cha Cambiasso

GK. Ismail Mpaki 2.Mohamed Omari 3 Isaya Ernest 4.Shabani Kingazi 5.Jackson Simba 6.Omary Hassa 7.Charlaes Masenga 8.Hija Shamte 9.Clement Kabela 10.Said Naushad 11.Manzi Limwinyi

Dakika ya kwanza - Simba Sc 0-0

Dakika ya 10 - Simba Sc 0-0 Cambiaso

Dakika ya 16 - Jimmyson anakosa goli baada ya kupiga shuti likidakwa na kipa Ismail mpaki wa Cambiaso

Dakika ya 19 - Beki Henock anatupatia goli la kwanza kwa kichwa akiunganisha mpira wa adhabu wa uliopigwa na Ibrahim Ajib

Dakika ya 24 - Cambiaso wanapata kona

Dakika ya 27 - Gadiel anajenga kibanda (Offside)

Dakika ya 30 - Simba wanapata faulo anapiga Ibrahim ajib mpira unaokolewa na beki wa Cambiaso

Dakika ya 31- Mabadiliko anatoka Beno Kakolanya anaingia Ally Salim

Dakika ya 33 - Ibrahim ajib analishika dimba vizuri akisaidia na Jonas Mkude na Bernard Morrison kwa pasi fupi fupi

Dakika ya 37 - Simba wanapata kona ikipigwa na Bernard Morrison mpira ukiokolewa na wachezaji wa Cambiaso

Dakika ya 43 - Ally Salim anadaka vizuri mpira wa mshambuliaji wa Cambiaso Clement baada ya kugongeana ndani ya boxi

Advertisement

Dakika 45- Mpira mapumziko Simba wakiwa mbele kwa bao 1-o goli likifungwa na mlinzi Henock Inonga

Kipindi cha pili - Mabadiliko upande wa SImba

Anatoka - Ibrahim Ajib, Gadiel Michael, Jonas Mkude na Said Norshad

Ameingia - Yussufu Mhilu, Saido Kanoute, Shomari Kapombe na Ambokile Mwaipopo

Dakika ya 46 Kipindi cha pili - Simba SC 1-0 Cambiaso

Dakika ya 54 - Yussufu Mhilu anakosa goli la wazi

Dakika ya 60 - Ally Salim anatoka anaingia Jeremiah Kisubi

Dakika ya 65 - Cambiaso wanafanya mabadiliko anatoka Manzi Limwinyi anaingia Ahmed Fred

Simba wanafanya mabadiliko anatoka Mzamiru Yassin anaingia Abdul Swamad Kassim Ally

Dakika ya 68 - Cambiaso wanasawazishia kupitia kwa Clement Kabela

Dakika ya 70 - Simba SC 1-1 Cambiaso

Dakika ya 77 - Mpira unachezwa kati kati ya uwanja huku wakishambuliana kwa zamu

Dakika ya 85 - Cambiaso wanakosa goli la wazi baada ya mabeki wa Simba kujichanganya

full Time - Simba SC 1-1 Cambiaso

Back to homepage
Share this story