Simba Sports Club
News

Kwaheri nahodha Violeth Nicholaus

15 Jul 2025

Violeth amejiunga nasi msimu wa 2018 akitokea Kigoma Sisters ambapo kabla ya hapo amepitia timu ya Evergreen Queens.

Katika kipindi cha miaka miaka saba amekuwa mchezaji tegemezi pamoja na kiongozi wa timu uwanjani.

Violeth ameiongoza Simba Queens kushinda mataji ya Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania (TWPL) katika misimu ya:

2019/2020

Advertisement

2020/2021

2021/2022

2023/2024

Akiwa ndani ya kikosi cha Simba Queens Violeth ameshiriki michuano ya Cecafa mara tatu pamoja na Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo alifika hatua ya nusu fainali.

Back to homepage
Share this story