Simba Sports Club
News

Kwaheri Freddy Michael Kouablan

22 Aug 2024

Fredy alijiunga nasi msimu uliopita katika usajili wa dirisha dogo na kufanikiwa kufunga mabao tisa katika mashindano yote.

Mwanzoni mwa msimu huu Fredy alikuwa sehemu ya mpango wa timu yetu lakini kiwango chake hakikumridhisha Mwalimu Fadlu Davids na hivyo kutoa pendekezo la kusajiliwa mshambuliaji mwingine ili kuboresha safu ya ushambuliaji

Advertisement

Tayari Fredy ameshaondoka Nchini Tanzania na kuelekea Algeria kuanza majukumu yake mapya.

Uongozi wa Simba unamtakia kila la heri mchezaji huyo katika majukumu yake mapya.

Back to homepage
Share this story