Simba Sports Club
News

Kocha Fadlu aongoza mazoezi kwa mara ya kwanza

11 Jul 2024

Fadlu ametua kambini jana jioni akiwa na wasaidizi wake na moja kwa moja leo ameanza kukiongoza kikosi kuelekea msimu mpya wa mashindano.

Katika mazoezi ya leo wachezaji walianza kukimbia uwanja mara kadhaa ili kurejesha utimamu wa mwili kutokana na kutoka kwenye mapumziko.

Advertisement

Baada ya zoezi hilo wachezaji walifanya mazoezi mbalimbali ya kucheza mpira uwanjani huku wakipewa maelekezo kutoka kwa Fadlu na wasaidizi wake.

Back to homepage
Share this story