Simba Sports Club
News

Kikosi kitakachotuwakilisha dhidi ya Mamelodi leo

9 Nov 2022 By simbasc 314 views
Kikosi chetu leo kitacheza Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Mamelodi Sundowns utakaopigwa katika mji wa Rabat saa moja usiku kwa saa za nyumbani Tanzania. Kocha Charles Lukula amefanya mabadiliko matatu ya kikosi kwa kuwaanzisha Vivian Corazone, S'arrive Lobo na Koku Ally ambao hawakuanza kwenye mchezo uliopita dhidi ya Green Buffaloes. Nyota Pambani Kuzoya, Olaiya Barakat na Amina Hemed ambao mchezo uliopita walianza leo wameanzia benchi. Kikosi kamili kilivyopangwa Gelwa Yona (21), Fatuma Issa (5), Diana Mnali (15), Daniela Kanyanya (22), Violet Nicholas (26), Joelle Bukuru (18), Vivian Corazone (4), S’arrive Lobo (2), Koku Ally (19), Opa Clement (7)Asha Djafari (24). Wachezaji wa Akiba Zubeda Mohamed (20), Janeth Simba (1), Dotto Evarist (11), Wema Maile (3), Jackline Albert (16), Topister Situma (13), Pambani Kuzoya (17), Amina Hemedi (14), Olaiya Barakat (9).
Advertisement
Back to homepage
Share this story