Kabla ya kuondoka kikosi kimefanya mazoezi ya mwisho asubuhi katika Uwanja wetu wa Mo Simba Arena tayari kwa mchezo huo.
Tumeondoka na kikosi kamili kuelekea Morogoro ambapo hakuna mchezaji yoyote ambaye amesalia isipokuwa nahodha John Bocco anayeendelea kuuguza majeraha.
Advertisement
Kwa sasa kila mchezo tumeupa umuhimu mkubwa na alama tatu ndio malengo yetu, tunafahamu Prisons ipo kwenye kiwango bora kwa sasa lakini tumejipanga kuwakabili.