Simba Sports Club
News

Kikosi kamili chaanza mazoezi

11 Jun 2022

Kikosi kilianza mazoezi tangu Juni 6 kwa wachezaji ambao hawakuwa katika majukumu ya timu za taifa lakini leo kimekamilika na wote wamejumuika.

Maandalizi ya mchezo wetu wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Mbeya City utakaopigwa Juni 16 yanaendelea vizuri na kila kitu kipo sawa.

Advertisement

Morali ya wachezaji ipo juu na kila mmoja amejitahidi kuonyesha jitihada mazoezini ili kulishawishi benchi la ufundi kumuamini.

Back to homepage
Share this story