Simba Sports Club
News

Kibu afanya maajabu jioni kwa Mkapa

15 Dec 2024

Kibu amefunga bao hilo dakika ya mwisho ya nyongeza baada ya kumalizia mpira wa krosi uliopigwa na kiungo mkabaji, Yusuph Kagoma.

Mshambuliaji Hazem Haj Hansen aliipatia CS Sfaxien bao la kwanza dakika ya tatu baada ya mlinzi Che Fondoh Malone kurudisha pasi fupi kwa mlinda mlango.

Kibu alitupatia bao la kusawazisha kwa kichwa dakika ya nane baada ya kumalizia mpira wa adhabu uliopigwa na Jean Charles Ahoua.

Kipindi cha pili tuliongeza kasi huku Sfaxien wakitumia muda mwingi kujiungusha na kupoteza muda.

Mabadiliko aliyofanya kocha Fadlu Davids kipindi cha pili ya kuwaingiza Valentine Nouma, Kagoma, Joshua Mutale na Steven Mukwala yaliongeza kasi na kutufanya kuongeza mashambulizi mengi langoni mwa Sfaxien.

Advertisement

X1. Camara, Kapombe, Zimbwe Jr (Nouma 77'), Che Malone (Chamou 64'), Hamza, Fernandez (Kagoma 64'), Kibu, Ngoma, Ateba (Mukwala 45'), Ahoua (Mutale 64'), Awesu

Walioonyeshwa kadi: Che Malone 57' Kibu 90+9

X1: Aymen, Nasraoui (Koume 45'), Conte, Hazem (Habboubi 55'), Achref (Baraket 55'), Derbali, Pedro, Dhaoui (Becha 71'), Baccar, Sakouhi (Traore 71') Layouni

Walioonyeshwa kadi: Habboubi 63' Aymen 66'

Back to homepage
Share this story