Simba Sports Club
News

Kelvin Kijili ni Mnyama

12 Jul 2024

Kijili mwenye umri wa miaka 24 ni kijana mwenye kipaji na kasi amekuwa akitumika kuanzisha mashambulizi kutokea upande wa kulia.

Akiwa na Singida Fountain Gate msimu uliopita Kijili amesaidia kupatikana kwa mabao manne (assist).

Kijili amekuja kuongeza kitu kikubwa kwenye kikosi chetu na kutokana na umri alionao tunaamini ataendelea kuwa msaada kwa timu kwa muda mrefu.

Advertisement

Usajili tuliofanya kuelekea msimu mpya wa mashindano tumezingatia kigezo cha umri kwakuwa malengo yetu ni kujenga timu imara ya muda mrefu.

Tayari Kijili amejiunga na wenzake kambini nchini Misri kuendelea na maandalizi ya msimu mpya wa mashindano 2024/25.

Back to homepage
Share this story