Matola amesema kikosi kimefanya mazoezi kwa wiki mbili na kimekamilika baada ya wale waliokuwa kwenye majukumu ya timu za taifa kujiunga pamoja na wenzao.
Matola ameweka wazi kuwa sisi ni timu kubwa na tunahitaji kushinda kila mchezo uliopo mbele yetu ikiwemo wa kesho bila kujali tunapambania ubingwa au la.
Advertisement
"Tuko tayari kwa mchezo wa kesho mchezo wa kesho, wachezaji wapo kwenye hali nzuri maandalizi yamekamilika na tuna imani tutapata alama zote tatu.
"Tunaiheshimu Mbeya City, inatupa ushindani mkubwa tukikutana nayo lakini tupo tayari kukabiliana nao kulingana na maandalizi tuliyofanya," amesema Matola.