Simba Sports Club
News

Karibu Unyamani Lameck Lawi

20 Jun 2024

Lawi ni kijana mwenye kipaji kikubwa na amekuwa ngome imara kwenye kikosi cha Coastal msimu uliopita na hicho ndicho kilichotuvutia kumsajili.

Usajili wa Lawi ni mkakati wa kuijenga Simba mpya yenye ushindani kuelekea msimu wa mashindano wa 2024/25.

Advertisement

Lawi mwenye umri wa miaka 18 na umbile refu anakuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa katika kikosi chetu kuelekea msimu mpya wa Ligi.

Lameck Lawi licha ya umri wake mdogo lakini ni Mlinzi mwenye uwezo mkubwa aliyewavutia wapenzi wa mpira nchini Tanzania na nje ya mipaka ya Nchi yetu na usajili wake tunategemea ataongeza kitu kikubwa katika kikosi akisaidiana na walinzi wazoefu waliokuwepo.

Back to homepage
Share this story