Precious raia wa Nigeria mwenye miaka 22 amejiunga nasi akitokea Yanga Princess kwa mkataba wa miaka miwili.
Msimu uliopigwa Precious amefunga mabao matatu na kusaidia kupatikana kwa jingine moja na alikuwa mchezaji muhimu wa kikosi cha kwanza kwenye timu yake.
Advertisement
Msimu ujao tumedhamiria kufanya vizuri kwenye michuano ya ndani na ile ya kimataifa ndio maana tunasajili wachezaji bora.
Precious ni mchezaji mzoefu wa ligi ya ndani pamoja na michuano ya Kimataifa.