Camara 23, ana uwezo mkubwa wa kucheza kama mlinzi wa kushoto na kiungo mkabaji hiyo ni moja ya sifa iliyotuvutia kuinasa saini yake.
Msimu uliopita Camara alikuwa akicheza Al Waab ya Qatar na kabla ya hapo alikuwa akikipiga CS Sfaxien ya Tunisia.
Advertisement
Tayari Camara amejiunga na kambi ya maandalizi inayoendelea nchini Misri na alikuwepo kwenye kikosi kilichoibuka na ushindi wa mabao 2-0 katika mechi ya kirafiki dhidi ya Karhaba SC wikiendi iliyopita.