Nyota hao wamekuwa na takwimu bora zaidi kulinganisha na wengine ambapo mlinda mlango Aishi Manula na nahodha John Bocco walikuwepo katika tano bora.
Katika mwezi Februari Kapombe amecheza mechi nne akifunga bao moja na kusaidia kupatikana kwa mengine mawili.
Inonga amecheza mechi zote sita za mwezi Februari wakati Banda akicheza nne akifunga bao moja na kusaidia kupatikana kwa moja pia.
Advertisement
Zoezi la kupiga kura litaanza leo saa 10 jioni kupitia Tovuti yetu ya www.simbasc.co.tz na kumalizika Jumatano Machi 2, saa 10 jioni.
Mshindi atakabidhiwa fedha taslimu Sh 2,000,000 na tuzo kutoka kwa wadhamini Emirate Aluminium ACP kama zawadi ya kuibuka kidedea.