Simba Sports Club
News

Kanoute, Bwalya, Dilunga wachuana Mchezaji Bora Simba

1 Nov 2021 By simbasc 5,437 views

Nyota watatu wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwania tuzo ya mchezaji bora wa Oktoba wa mashabiki ya Emirate Aluminium ACP Simba Fans Player of the Month.

Emirate Aluminium ACP wamekuwa na utaratibu wa kutoa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi kwa ajili ya kuongeza hamasa kwa wachezaji.

Wachezaji hao ni viungo Sadio Kanoute, Rally Bwalya na Hassan Dilunga ambao wamekuwa kwenye kiwango bora katika mwezi huo.

Awali walikuwa wachezaji watano akiwamo mlinda mlango Aishi Manula na Bernard Morrison kabla ya Kamati maalumu kuwachuja na kubaki na hao watatu ambao wameingia fainali.

Advertisement

Mshindi kati ya watatu hao atapatikana kupitia kura za mashabiki zitakazopigwa katika tovuti rasmi ya klabu ya www.simbasc.co.tz

Zoezi la kupiga kura limeanza leo na litakamilika Jumatano saa 10 jioni na mshindi atakabidhiwa fedha taslimu Sh 2,000,000 kutoka kwa wadhamini Emirate Aluminium ACP.

[totalpoll id="6341"]
Back to homepage
Share this story