Mara kadhaa Kagere amekuwa akitokea benchi lakini leo Kocha Seleman Matola ameamua kumuanzisha kuongoza mashambulizi.
Kagere atapata msaada wa karibu kutoka kwa viungo washambuliaji Pape Sakho na Peter Banda ambao watatokea pembeni huku Kibu Denis akicheza namba 10.
Mlinda mlango Beno Kakolanya ataendelea kusimama kwenye milingoti mitatu kulifanya lango letu kuwa salama.
Kikosi kamili kilichopangwa
Beno Kakolanya (30), Jimmyson Mwanuke (21), Gadiel Michael (2), Kennedy Juma (26), Pascal Wawa (6), Erasto Nyoni (18), Pape Sakho (10), Sadio Kanoute (13), Medie Kagere (14), Kibu Denis (38), Peter Banda (11).
Wachezaji wa Akiba
Ally Salim (1), Joash Onyango (16), Henock Inonga (29), Taddeo Lwanga (4), John Bocco (4), Hassan Mussa (52) , Shafih Hassan 53, Kassim Omary 55, Yusuf Mhilu (27).