Simba Sports Club
News

Israel Patrick ni Mwekundu

16 Aug 2021 By simbasc 3,131 views

Mlinzi wa kulia Israel Patrick Mwenda, amejiunga na kikosi chetu akitokea Timu ya Manispaa ya Kinondoni (KMC).

Mwenda amekuwa kwenye kiwango bora msimu uliopita akiwa KMC hali iliyosababisha kulivutia benchi la ufundi chini ya Kocha Didier Gomes.

Licha ya uwezo mkubwa alioonyesha msimu huu pia umri wa Mwenda ni mdogo ambao unamruhusu kucheza soka kwa muda mrefu.

Advertisement

Mwenda anakuwa mchezaji wa tano kusajiliwa ndani ya kikosi chetu baada ya Peter Banda aliyetoka Big Bullet ya Malawi, Yusuph Mhilu kutoka Kagera Sugar, Duncan Nyoni, Ousmane Sakho na Henock kutoka DC Motema Pembe.

Bado tunaendelea kufanya usajili kwa umakini mkubwa kulingana na mapendekezo ya benchi la ufundi kabla ya kuanza msimu mpya wa ligi 2021/22.

Back to homepage
Share this story