Mpaka mzunguko wa kwanza unakamilika Februari 15 ukijumuisha mechi tisa, Queens tumeshinda tisa na kutoka sare moja na kupoteza moja.
Nahodha wetu Opa Clement ndiye kinara wa ufungaji ambapo mpaka sasa amefunga mabao tisa huku Jentrix Shikangwa akifunga saba, Asha Djafar akifunga manne.
Takwimu za Queens Mzunguko wa kwanza wa SLWPL
Mechi Ushindi Kupoteza Sare Mabao
Advertisement
9 7 1 1 29
Uwiano wa mabao yetu ni 24 kwa kuwa tumeruhusu matano pekee.
Mchezo wetu wa kwanza wa mzunguko wa pili wa SWPL utakuwa Machi 8 dhidi ya JKT Queens utakaopigwa Uwanja wa Meja Genarali Isamuhyo.
Mchezo dhidi ya JKT Queens ni wa kisasi kwetu kwa kuwa walitufunga bao moja katika mchezo wa kwanza wa ufunguzi wa ligi.