Meneja Habari na Mawasiliano Ahmed Ally amesema lengo la kuweka hadharani viingilio ni kuwapa nafasi mashabiki kununua mapema ili kuepuka usumbufu.
Ahmed amesema mwaka jana tiketi za Simba Day ziliisha siku mbili kabla ya tamasha lakini safari hii tumepanga ziishe siku tano kabla.
"Kikubwa mashabiki nunueni tiketi mapema ili kuepuka usumbufu, Simba hii sio ya kuitazama kwenye TV. Tiketi zitaisha mapema kwahiyo Wanasimba msichelewe kununua," amesema Ahmed.
Hivi hapa Viingilio vyenyewe:
Mzunguko Sh. 5000
Advertisement
Machungwa Sh. 10,000
VIP C Sh. 20,000
VIP B Sh. 30,000
VIP A Sh. 40,000
Platinum Sh. 200,000