Simba Sports Club
News

Hivi hapa viingilio vya mchezo wetu dhidi ya Raja Casablanca

12 Feb 2023 By simbasc 351 views
Kiingilio cha chini ya mchezo wetu wa pili wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Raja Casablanca utakaopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Februari 18 kitakuwa Sh. 5000. Viingilio vimetangazwa mapema ili kuwapa nafasi mashabiki kununua mapema sababu tunahitaji mashabiki wajitokeze kwa wingi uwanjani kuipa sapoti timu. Viingilio ni kama ifuatavyo: Mzunguko Sh. 5000 VIP B & C Sh. 20000 VIP A Sh. 30,000 Platinum Sh. 100,000 Platinum Plus Sh. 150,000 Vitu ambavyo atavipata atayenunua tiketi za Platinum ni. 1. Escort kutoka Hoteli ya Hyatt Regency mpaka uwanjani. 2. Kifurushi maalum kutoka Simba. 3. Chakula na Vinywaji ukiwa uwanjani. Ili kupata tiketi za Platnum na Platnum Plus tupigie kwa namba hii +255742771311. Tayari tiketi zimeanza kuuzwa kwa njia ya mtandao muda mfupi ujao tutatangaza vituo ambavyo zitapatikana.
Advertisement
Back to homepage
Share this story