Bonanza la Simba Day litafanyika Jumamosi ya Septemba 5 katika Viwanja vya Mwembe Yanga Temeke Dar es kuanzia saa nne asubuhi.
Matawi 22 yamethibitisha kushiriki na kila mmoja tayari ameshafahamu atacheza na nani kwenye mechi ya kwanza baada ya droo kukamilika.
Hii hapa ratiba kamili iliyopangwa baada ya kukamilika kwa droo.
1. Simba Hatari vs Home Boys (Wazo Hill)
2. Wababe wa Kimataifa vs Simba Maendeleo (Lumo)
3. Wekundu wa Kibamba vs Wekundu wa Mtogole
4. Mpira Maendeleo vs Simba Damu Fans (SDF)
5. Mpira Pesa Group vs Wekundu wa Chamazi
6. Vuvuzela vs Nguvu ya Simba Asilia
7. Wakwanza Sisi (Mbagala) vs Wekundu wa Terminal
8. Mpira Pesa Mikumi vs Karume Unstoppable
9. Ukonga Mazizini vs Kapu la Magoli
10. KRM vs Tunawakera
11. Asili ya Simba (Kawe) vs Mtongani
Bingwa wa Tembo Card Simba Matawi Bonanza atajinyakulia pesa taslimu Shilingi milioni mbili (2,000,000) Kombe pamoja na medali wakati mshindi wa pili akijipatia Shilingi milioni moja (1,000, 000) na medali.