Dakika ya kwanza - Telecom 0-0 Simba SC
Dakika ya 10 - Mechi inaendelea kila timu ikipiga pasi haswa upande wake.
Dakika ya 15 - Shuti la Karabaka linatolewa na kipa wa Telecom na kuwa kona
Dakika ya 18 - Telecom wanapata bao la kuongoza lililofungwa kwa kichwa na Ashour Shika, aliyeunganisha mpira wa krosi.
Dakika ya 30 - Mapumziko mafupi (Water Break)
Dakika ya 35 - Mchezo unaendelea tumerudi kwa kasi
Dakika ya 42 - Karabaka anapoteza nafasi ya wazi akiwa ndani ya boksi baada ya kupiga shuti lililotoka nje. Karabaka alikutana uso kwa uso na na kipa wa Telecom Karabaka alipokea pasi kutokea kwa Hamza.
Mapumziko - Telecom 1-0 Simba
Kipindi Cha pili kimeanza - Telecom 1-0 Simba mabadiliko anatoka David Kameta anaingia Kelvin Kijili
Dakika ya 47 - Kipindi cha pili kimeanza kwa kasi
Dakika ya 53 - Krosi safi ya Kijili anamkuta, Fredy ndani ya boksi akiunganisha kwa mguu wa kulia na kipa wa Telecom anapangua na kuwa
Dakika ya 58 - Mabadiliko anatoka Freddy anaingia Valentino Mashaka
Dakika ya 62 - Shambulizi zuri kutokea nyuma linamkuta, Nouma aliyekuwa pembeni kushoto na kupiga krosi nzuri ya chinichini na kumkuta, Mashaka aliyefunga bao la kusawazisha.
Mabadiliko Anatoka - Okejepha na Anaingia - Awesu Awesu
Dakika ya 65 - Mchezo unaendelea Telecom 1-1 Simba
Dakika ya 71 - Mabadiliko Anatoka - Chasambi Anaingia - Onana
Dakika ya 78 - Mechi inaendelea tunawapelekea mashambulizi, Telecom na tunamiliki mpira muda mwingi huku Telecom wakionekana kupoteza muda.
Dakika ya 80 - Mpira unaendelea huku tukiwashambulia Telecom wamepaki basi
Dakika 87. Anatoka - Nouma na Anaingia - Chasambi
Dakika ya 88 - Krosi nzuri ya Kijili inamkuta Chasambi aliyekuwa ndani ya boksi na kuunganisha kwa (Semi-Volley) na kufunga bao la pili.
Mpira umemaliza - Telecom 1-2 Simba