Simba Sports Club
News Videos

Fetty Densa: Nyota wapya wamezoea mazingira haraka

15 Nov 2023

Fetty Densa amesema ukifika mazoezini huwezi kutambua nani mgeni kwakuwa wote wapo sawa.

Densa ambaye ana uwezo mkubwa wa kucheza nafasi nyingi kwa ufasaha uwanjani amesema kila mchezaji anajua umuhimu wa kutwaa ubingwa wa ligi msimu huu.

Advertisement

"Tunaendelea vizuri na mazoezi, tupo kwenye hali nzuri, morali zipo juu na jambo jema ni kwamba hata wenzetu wageni wamezoea haraka mazingira na tunashirikiana vizuri.

"Msimu uliopita hatukuwa na furaha kutokana na kukosa ubingwa uliotufanya kushindwa kushiriki michuano ya Klabu Bingwa sasa tumejipanga na tunataka kurudisha taji letu," amesema Fetty Densa.

Back to homepage
Share this story