Ngoma ameonyesha kiwango bora katika mechi zote sita za Kombe la Mapinduzi tulichoza.
Katika mechi hizo sita Ngoma alichaguliwa mchezaji bora wa mechi (Man of the Match) mara mbili.
Advertisement
Pamoja na mabadiliko ya kikosi yaliyokuwa yanafanywa na Kocha Abdelhak Benchikha, Ngoma amefanikiwa kucheza mechi zote.
Kuna mechi ambazo Benchikha alimtumia Ngoma kama kiungo mshambuliaji namba 10 na nyingine namba sita na wakati mwingine namba nane.