Che Malone alishindwa kuendelea na mchezo na kutolewa dakika ya 20 baada ya kupata maumivu hayo.
Daktari wa timu, Edwin Kagabo amesema baada ya majibu ya vipimo kutoka ndio itajulikana ameumia kwa kiasi gani na matibabu yake yatakuwaje.
Advertisement
"Che Malone alipata maumivu kwenye mguu na kushindwa kuendelea na mchezo, leo amefanyiwa vipimo na tunasubiri majibu ili kufahamu ukubwa wa jeraha na matibabu yake yatakavyokuwa," amesema Dk. Kagabo.