Simba Sports Club
News

Bodi ya Wakurugenzi wapigwa msasa

9 Jun 2023 By simbasc 210 views
Uongozi wa klabu leo umeendesha mafunzo ya uongozi kwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi yaliyolenga kujenga taasisi bora yenye weledi na kufikia dira yetu ya kuwa moja ya klabu bora barani Afrika. Mafunzo hayo yameongozwa na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Wakurugenzi, Said Kambi Shaaban. Wajumbe walioshiriki ni Mwenyekiti wa Bodi, Salim Muhene, Mwenyekiti wa klabu, Murtaza Mangungu na Mtendaji Mkuu wa Klabu, Imani Kajula. Wengine ni Wajumbe wa Bodi, Asha Baraka, Issa Masoud, Seleman Haroub, Dkt. Muba Seif, Raphael Chegeni na Dkt. Rodney Chiduo.
Advertisement
Back to homepage
Share this story