Chilunda ni mchezaji kijana mwenye kiwango bora ambaye alijiunga na Simba msimu uliopita kwa mkataba wa mwaka mmoja wenye nafasi ya kuongezwa kama tungeridhishwa na kiwango chake
Katika dirisha la mwezi Januari Chilunda alicheza kwa mkopo KMC hadi mwisho wa msimu lakini sasa hayupo kwenye mipango ya timu yetu kuelekea msimu ujao.
Advertisement
Simba inaamini katika uwezo wa Chilunda na inamtarajia kufanya makubwa katika timu ambayo itamsajili.
Tunamtakia kila la kheri Chilunda katika maisha yake mapya nje ya klabu ya Simba.