Simba Sports Club
News

Alichosema Zoran baada ya mchezo dhidi ya Kagera

21 Aug 2022 By simba 841 views

Kocha Mkuu Zoran Maki, ameweka wazi amefurahi kupata alama tatu katika mchezo wa jana dhidi ya Kagera Sugar ingawa amekiri tumepoteza nafasi nyingi.

Zoran amesema tumepoteza nafasi nane kipindi cha kwanza na sita kupindi cha pili na mpira kumalizika kwa ushindi wa mabao mawili kitu ambacho si kizuri.

Advertisement

Zoran ameongeza kuwa amefurahi kuona wachezaji wapya wawili, Moses Phiri na Dejan Georgijevic wakifunga katika mchezo wa jana kitu ambacho kinawapa hali ya kujiamini.

"Nimefurahi kupata alama tatu kwenye mchezo wa jana, tulimiliki sehemu kubwa ya mchezo lakini tulipoteza nafasi nyingi ambazo zingetufanya kupata ushindi mnono zaidi.

"Tuna wiki moja na nusu ya kujiandaa kabla ya mchezo wetu unaofuata naamini tutafanya marekebisho," amesema Kocha Zoran.

Back to homepage
Share this story