Simba Sports Club
News

'Acrobatic' ya Sakho bao bora la wiki CAF

16 Feb 2022 By simbasc 1,637 views

Bao la 'tiktak' la kiungo mshambuliaji Pape Sakho 'acrobatic' alilofunga dhidi ya ASEC Mimosas katika mchezo wetu wa hatua ya makundi limechaguliwa bao bora la wiki la Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF).

Sakho alifunga bao hilo dakika ya 12 akimalizia mpira wa krosi uliopigwa na mlinzi wa kulia Shomari Kapombe.

Advertisement

Katika mchezo huo uliopigwa Jumapili iliyopita Uwanja wa Benjamin Mkapa, Sakho alionyesha kiwango safi ingawa alishindwa kuendelea na mechi kutokana na kupata maumivu ya mguu.

Back to homepage
Share this story