Jentrix akabidhiwa kiatu cha ufungaji bora SLWPL

Mshambuliaji Jentrix Shikangwa amekabidhiwa tuzo yake ya mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Wanawake ya Serengeti Lite Women’s Premier League (SLWPL) 2022/23.

Shikangwa amekabidhiwa kiatu cha dhahabu katika hafla ya tuzo za TFF 2022/23 zinazofanyika jijini Tanga usiku huu.

Shikangwa pia amechaguliwa katika kikosi bora cha SLWPL msimu wa 2022/23.

Wachezaji wengine walioingia kwenye kikosi bora cha msimu ni pamoja na walinzi Fatuma Issa ‘Fetty Densa’ na Violeth Nicholas.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER