Bocco kuongoza mashambulizi dhidi ya Jwaneng Galaxy

Nahodha John Bocco ataongoza mashambulizi dhidi ya Jwaneng Galaxy katika mchezo wa hatua ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika utakaopigwa Uwanja wa Taifa wa Botswana saa 10 jioni.

Bocco atapata msaada wa karibu kutoka kwa viungo washambuliaji Bernard Morrison, Hassan Dilunga na Rally Bwalya.

Mlinzi wa kati Henock Inonga amepangwa kusimama na Pascal Wawa huku kiungo Sadio Kanoute aliyekuwa majeruhi akirejea moja kwa moja kikosini.

Kikosi Kamili kilivyopangwa.

Aishi Manula (28), Shomari Kapombe (12), Mohamed Hussein (15), Pascal Wawa (6), Henock Inonga (29), Taddeo Lwanga (4) Bernard Morrison (8) Sadio Kanoute (13), John Bocco (22), Rally Bwalya (8), Hassan Dilunga (24).

Wachezaji wa Akiba

Beno Kakolanya (30), Peter Banda (11), Erasto Nyoni (18), Duncan Nyoni (23), Mzamiru Yasin (19),
Israel Patrick (5), Joash Onyango (16), Medie Kagere (14), Kennedy Juma (26).

SHARE :
Facebook
Twitter

One Response

  1. Pingback: Homepage

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER