Jumapili Februari 13 tutashuka katika Uwanja wa Benjamin Mkapa saa 10 jioni kuikabili ASEC Mimosas kutoka Ivory Coast katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika na tayari viingilio vimetangazwa.
Maandalizi ya mchezo yanaendelea vizuri ambapo viingilio hivyo ni kama ifuatavyo;
Mzunguko Sh 5,000
VIP B na C Sh 20,000
VIP A Sh 40,000
Tiketi tayari zimeanza kuuzwa leo kupitia mitandao ya simu na Jumatano tutatangaza vituo ambavyo tiketi zitapatikana.
One Response