Dirisha la Usajili limefunguliwa Jumamosi iliyopita nasi tunaendelea kufanya maboresho kikosi chetu ambacho tunategemea kukitumia katika msimu wa Ligi 2023/24.
Tayari Kitengo cha Habari na Mawasiliano chini ya Ahmed Ally wamepokea mafaili ya wachezaji ambao tumefanikiwa kuwasajili kwa ajili ya kuwatambulisha kwa Wanasimba siku chache zijazo.
Weka bundle, chaji simu, tulia sebuleni kwako kula popcorn subiria habari njema za furaha