Tumemaliza Mzunguko wa kwanza TWPL tukiwa kileleni

Mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania (TWPL) umemalizika huku kikosi cha Simba Queens kikiwa kileleni mwa msimamo.

Ligi ya Wanawake ambayo inashirikisha timu 10 imesimama kupisha maandalizi ya timu ya Taifa ya Twiga Stars kujiandaa na michuano ya kufuzu Olimpiki dhidi ya Afrika Kusini ‘Banyana Banyana’.

Simba Queens imemaliza mzunguko huo ikiwa na alama 25 baada ya kucheza mechi tisa ikishinda nane na kutoka sare moja.

Katika michezo hiyo Queens imefunga mabao 33 huku ikiruhusu kufungwa mabao matano.

Matokeo ya mechi zote tisa za Simba Queens

Simba Queens 5 – 0 Ceassia Queens

Simba Queens 5 – 2 baobab queens

Simba Queens 3 – 1 Yanga Princess

Simba Queens 3 – 0 JKT Queens

Amani Queens 2 – 3 Simba Queens

Bunda Queens 0 – 0 Simba Queens

Simba Queens 7 – 0 Alliance Girls

Fountain Gate Princess 0 – 4 Simba Queens

Geita Queens 0-3 Simba Queens

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER