Tumemaliza mechi ya mwisho nyumbani kwa ushindi

Mchezo wetu wa mwisho katika Uwanja wa nyumbani wa Benjamin msimu wa 2021/22 dhidi ya Mtibwa Sugar umemalizika kwa ushindi wa mabao 2-0.

Pape Sakho alitupatia bao la kwanza dakika ya 16 baada ya kumalizia pasi ya kisigino iliyopigwa na Kibu Denis.

Peter Banda alitupatia bao la pili dakika ya 44 baada ya kupiga shuti lililokwenda moja kwa moja na kumshinda mlinda mlango wa Mtibwa, Shaban Kado.

Kiungo wa Mtibwa Said Ndemla alitolewa kwa kuonyeshwa kadi nyekundu dakika ya 66 baada ya kumchezea vibaya Sadio Kanoute.

Kocha Seleman Matola alifanya mabadiliko ya kuwatoa Denis Kibu na Pape Sakho na Kuwaingiza Yusuf Mhilu na Taddeo Lwanga.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER