Tumechukua tatu za Mbeya City

Kikosi chetu kimefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa.

Tulianza mchezo kwa kasi na kuliandama lango la City tukitengeneza nafasi lakini ufanisi wetu katika eneo la mwisho haikuwa nzuri.

Pape Sakho alitupatia bao la kwanza dakika ya 38 kwa mkwaju wa penati baada kufanyiwa madhambi ndani ya 18 na mlinda mlango wa City, Haroun Mandanda.

Kipindi cha pili tulirudi kwa kasi ambapo dakika ya 55 Sakho alitupatia bao la pili baada ya kupokea pasi ndefu ya Mzamiru Yassin na kuwazidi mbio walinzi wa City kabla ya kumpiga chenga Mandanda.

Peter Banda alitupatia bao la tatu dakika ya 76 akimalizia pasi safi ya Yusuf Mhilu kufuatia shambulizi aliloanzisha mwenyewe.

Kocha Seleman Matola aliwatoa Sakho, Kibu Denis, Mzamiru na Bwalya na kuwaingiza Medie Kagere, Banda, Mhilu na Taddeo Lwanga.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER