Timu yarejea nyumbani salama

Kikosi chetu kimewasili salama jijini Dar es Salaam leo mchana kutoka nchini Morocco baada ya majukumu ya Kombe la Shirikisho Afrika hatua ya makundi kukamilika.

Baada ya kufika Dar wachezaji wameruhusiwa kwenda kuziona familia zao na kesho watarajea mazoezini kujiandaa na mechi ya Ligi Kuu ya NBC itakayopigwa Ijumaa Machi 4, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa saa moja usiku dhidi ya Biashara United.

Mechi hiyo ni muelendelezo wa ligi ambapo tutakuwa tunaanza rasmi mzunguko wa pili.

Katika mchezo huo tunatarajia uwepo wa baadhi ya wachezaji wetu ambao walikuwa majeruhi na kuikosa mechi kadhaa ambao watakuwa wamepona na wako fiti.

SHARE :
Facebook
Twitter

One Response

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER