Timu yaifuata Mbeya Kwanza Songea

Kikosi chetu kimeanza safari asubuhi hii kuelekea mjini Songea tayari kwa mchezo wa Jumatano wa kukamilisha msimu wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Mbeya Kwanza.

Kikosi kimeondoka jijini Mbeya baada ya mchezo wa jana kwa basi kikiwa na wachezaji wote tuliosafiri nao kwa ajili ya mechi mbili za Nyanda za Juu Kusini.

Baada ya timu kuwasili Songea wachezaji watafanya mazoezi ya utimamu wa mwili (recovery) baada ya mechi ya jana dhidi ya Tanzania Prisons na kesho tutafanya ya mwisho.

Mchezo wetu dhidi ya Mbeya Kwanza utapigwa Jumatano saa 10 jioni katika Uwanja wa Majimaji.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER