Timu yafanya mazoezi ya mwisho kabla ya kuivaa Kotoko kesho

Kikosi chetu leo kimefanya mazoezi ya mwisho usiku huu katika Uwanja wa Al Hilal kujiandaa na mchezo wa kesho dhidi ya Asante Kotoko kutoka Ghana.

Kikosi kimewasili hapa Khatoum jana mchana na jioni kilifanya mazoezi ya utimamu wa mwili kutokana na uchovu wa safari.

Wachezaji wote tuliosafiri nao wapo kwenye hali nzuri na hakuna ambaye tutamkosa kutokana na majeruhi.

Mchezo wetu wa kesho utapigwa katika Uwanja wa Al Hilal saa moja usiku ambapo kwa saa za nyumbani itakuwa saa mbili.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER