Timu kurejea Dar usiku huu

Baada ya ushindi wa mabao 3-0 tuliopata dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa Uwanja wa Manungu Complex kikosi kimeanza safari ya kurejea jijini Dar es Salaam.

Baada ya timu kufika wachezaji watapewa mapumziko ya siku moja ambapo watarejea mazoezini Jumatatu kuanza maandalizi ya mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Horoya FC kutoka Guinea.

Mchezo dhidi ya Horoya utapigwa Jumamosi Machi 18, katika Uwanja wa Benjamin Mkapa saa moja usiku.

Ushindi katika mchezo huo ndio utatupa tiketi ya kufuzu hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika ndio maana tunaupa umuhimu mkubwa.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER