Simba Klabu Bora Kidigitali mwaka 2021

Klabu yetu leo imekabidhiwa Tuzo ya Klabu Bora ya Kigitali kutokana na kufanya vizuri katika mitandao ya kijamii mwaka 2021.

Tuzo hiyo tumekabidhiwa na waandaaji Serengeti Byte baada ya kuzishinda timu nyingine zinazoshiriki Ligi Kuu ya NBC ambazo ni Azam FC, Mbeya City, Ruvu Shooting na Yanga.

Kwa mujibu wa Serengeti Byte, klabu yetu imekuwa na muendelezo mzuri katika Kitengo chetu cha Habari na Mawasiliano na tunafanya vizuri katika mitandao ya kijamii ikiwa na maana ya kwenda na wakati.

Mpaka sasa tunapatikana katika majukwaa mbalimbali katika mitandao ya kijamii ambayo ni Instagram, Facebook, Twitter na Tiktok.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER