Oppa kuongoza mashambulizi dhidi ya Lady Doves

Mshambuliaji kinara wa Simba Queens, Oppah Clement atakiongoza kikosi chetu katika mchezo wa pili wa Michuano ya Caf Women’s Champions League Cecafa Qualifier 2021 dhidi ya Lady Doves kutoka Uganda leo katika Uwanja wa Moi Kasarani.

Oppa amejiunga na wenzake juzi na alikosa mchezo wa kwanza dhidi ya PVP FC tulioibuka na ushindi wa mabao 4-1 kutokana na matatizo ya kifamilia ambayo yamemalizika na amerejea kikosini.

Oppa ndiye mfungaji bora wa kikosi chetu katika msimu uliopita wa ligi ya Wanawake ‘Serengeti Lite Women’s Champions League’ hivyo tunaamini atafanya vizuri kwenye mchezo wa leo.

Kikosi Kamili kilivyopangwa

  1. Zubeda Mongi
  2. Dotto Evarist
  3. Violeth Nicholaus
  4. Julieta Singano
  5. Fatma Issa
  6. Joelle Bukuru
  7. Danai Bhobho
  8. Zena Khamis
  9. Mawete Musolo
  10. Oppa Clement
  11. Ruth Kipoi

Wachezaji wa Akiba

Janeth Shija
Gelwa Yona
Maimuna Hamis
Silvia Thomas
Violeth Thadeo
Jackline Albert
Koku Kipanga
Aisha Juma
Shelda Boniface
Asha Kadosho

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER