Nyota tisa waitwa Taifa Stars

Wachezaji tisa kutoka kwenye kikosi chetu wameitwa katika Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayojiandaa na mchezo wa kufuzu Fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) dhidi ya Uganda.

Baada ya kuonyesha kiwango safi katika mechi za maandalizi ya msimu (Pre Season) mlinda mlango namba mbili Beno Kakolanya naye amejuimuishwa kikosini.

Kiungo mkabaji Jonas Mkude na mshambuliaji mpya Habib Kyombo nao ni miongoni mwa nyota 25 walioitwa na Kocha Kim Poulsen kwa ajili ya mechi hizo.

Wachezaji hao walioitwa ni walinda mlango

Aishi Manula
Beno Kakolanya

walinzi

Shomari Kapombe
Mohamed Hussein
Kennedy Juma

Viungo

Jonas Mkude
Mzamiru Yassin

Washambuliaji

Kibu Denis
Habib Kyombo

Stars itaingia kambini Jumapili na mchezo wa kwanza utapigwa Agosti 28 Uwanja wa Benjamin Mkapa na marudio itakuwa Septemba 3 jijini Kampala, Uganda.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER