Nyota 23 waliosafiri kuifuata Biashara

Kikosi cha wachezaji 23 kimefika salama mkoani Mara tayari kwa mchezo wetu wa kwanza wa ligi dhidi ya Biashara United utakaopigwa kesho Jumanne katika Uwanja wa Karume saa 10 jioni.

Timu iliondoka jana saa 12 kwa Ndege kuelekea jijini Mwanza kabla ya leo asubuhi kuanza safari ya kuja Mara.

Kikosi hicho hicho ndicho kitaenda kuikabili Dodoma Jiji katika mchezo wetu wa pili utakaopigwa Septemba 30, katika Uwanja wa Jamhuri jijini humo.

Kikosi Kamili kinachosafiri

Makipa

  1. Ally Salim
  2. Beno Kakolanya
  3. Aishi Manula

Walinzi

  1. Israel Patrick
  2. Shomari Kapombe
  3. Mohamed Hussein
  4. Pascal Wawa
  5. Henock Inonga Baka
  6. Kennedy Juma
  7. Erasto Nyoni

Viungo

  1. Mzamiru Yassin
  2. Rally Bwalya
  3. Pape Sakho
  4. Peter Banda
  5. Hassan Dilunga
  6. Duncan Nyoni
  7. Taddeo Lwanga
  8. Jimmyson Mwinuke

Washambuliaji

  1. Chris Mugalu
  2. John Bocco
  3. Medie Kagere
  4. Yusuph Mhilu
  5. Kibu Denis
SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER