Simba leo imeanza mazoezi katika Uwanja wa Boko Veterans kujiandaa na mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Jwaneng Galaxy utakaopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Jumapili Oktoba 24.
Baada ya mazoezi ya jioni kikosi kimeingia kambini moja kwa moja tayari kwa maandalizi ya mchezo huo ili kufuata programu za mwalimu.