Simba Sports Club
Uncategorized

Timu kuondoka mchana kuifuata Mtibwa Moro

20 Jan 2022 By simbasc 678 views

Kikosi chetu kitaondoka leo mchana kuelekea mkoani Morogoro tayari kwa mchezo ujao wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa Jumamosi Uwanja wa Manungu.

Kabla ya kuondoka kikosi kilifanya mazoezi katika viwanja vyetu vya Mo Simba Arena ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mchezo huo.

Advertisement

Wachezaji wetu wawili Jonas Mkude na Kibu Denis hawatakuwa sehemu ya kikosi kutokana na kuendelea kuuguza maumivu waliyopata katika mchezo uliopita dhidi ya Mbeya City.

Back to homepage
Share this story