Simba Sports Club
Uncategorized

Fabrice Ngoma Mchezaji bora Kombe la Mapinduzi

13 Jan 2024 By simbasc 290 views
Kiungo mkabaji Fabrice Ngoma amechaguliwa mchezaji bora wa michuano ya Kombe la Mapinduzi mwaka 2024. Ngoma ameonyesha kiwango bora katika mechi zote sita za Kombe la Mapinduzi tulichoza. Katika mechi hizo sita Ngoma alichaguliwa mchezaji bora wa mechi (Man of the Match) mara mbili. Pamoja na mabadiliko ya kikosi yaliyokuwa yanafanywa na Kocha Abdelhak Benchikha, Ngoma amefanikiwa kucheza mechi zote. Kuna mechi ambazo Benchikha alimtumia Ngoma kama kiungo mshambuliaji namba 10 na nyingine namba sita na wakati mwingine namba nane.
Advertisement
Back to homepage
Share this story