Simba Sports Club
Uncategorized

Simba kuanza hatua ya kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika

13 Aug 2021 By simbasc 4,007 views

Shirikisho la Soka Afrika (CAF), limeitaja Simba kuwa miongoni mwa timu 10 ambazo hazitaanza hatua ya awali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

CAF imeweka wazi majina ya timu 54 ambazo zitashiriki michuano hiyo msimu huu huku timu yetu ikiwa miongoni mwa zile ambazo zitaanza hatua ya kwanza.

Advertisement

Hii ni mara ya kwanza kwetu kuanzia hatua ya kwanza kutokana na mafanikio tuliyopata msimu uliopita kwa kufanikiwa kufika robo fainali ya michuano hiyo.

Timu nyingine ambazo hazitacheza hatua ya awali ni Wydad Casablanca, Raja Casablanca, Zamelek, Al Ahly, ES Tunis, Esente Setif, Horoya, Mamelod na TP Mazembe.

Back to homepage
Share this story